Fiesta

Fiesta

Voda

Voda

Nunua

Nunua

Tuesday, October 4, 2016

COCA-C0LA ILVYOPATA JINALAKE


Coca-Cola ni moja ya kampuni maarufu duniani, ambayo hutengenezwa soda maarufu ya Coke na vinywaji vingine vya soda. Lakini, ilikuwaje hadi ikawa na jina hilo?

Labda umewahi kusikia kwamba Coca-Cola wakati mmoja ilikuwa na kiungo cha kusisimua ambacho kiliwafanya wateja kulipenda sana. Hii ni moja ya vilivyochangia jina lake.

"Coca", kwa Kiswahili koka, ni jina la jani la mmea wa koka, moja ya viungo ambavyo mvumbuzi wa kinywaji hicho, mwanakemia wa Atlanta John Stith Pemberton, alichanganya na shira kutengeneza kinywaji chake.

Majani ya koka hutumiwa kutengeneza kokeini.

Wakati huo, mwishoni mwa karne ya 19, ilikuwa kawaida kwa majani ya koka kuchanganywa na divai na kuwa kinywaji cha kuchangamsha mwili.

    Kokeini yagundulika kwenye kiwanda cha Coca-Cola

Kinywaji kipya alichotengeneza Pemberton kilikuwa njia nzuri ya kukwepa sheria zilizoharamisha uuzwaji wa pombe.

Sehemu hiyo nyingine ya jina Coca-Cola inatokana na kiungo kingine chenye nguvu, ingawa si maarufu sana.

Kiungo hiki ni kola.

Ganda ambalo huwa na kokwa za kola ndani yake huwa na urefu wa inchi mbili na kabla ya kukauka, huwa za rangi ya kijani.

Ndani yake huwa na sehemu yenye fundo za rangi nyekundu au nyeupe kabla hazijakauka.

Asili ya kola ni Afrika Magharibi na zimekuwa zikitafunwa kwa miaka mingi na wenyeji kama kitu cha kuchangamsha mwili.

Kokwa hicho huwa na kafeini na theobromine, ambavyo hupatikana pia kwenye chai, kahawa na kakao. Zina pia sukari na kolanin, ambayo huaminika kuwa kichangamsha moyo.

Kufikia karne ya 19, kola zilianza kusafirishwa Ulaya na Marekani na zikaanza kutumiwa katika tembe zilizokusudiwa kutumiwa kuongeza nguvu mwilini.
Papa Leo XIII

Muda si muda, zilianza kutumiwa kwenye vinywaji. Kinywaji kimoja maarufu kilikuwa Vin Mariani, cha Ufaransa kilichotayarishwa kwa kuchanganya maji ya coca na divai nyekundu.

Kilitengenezwa na mwanakemia Mfaransa Angelo Mariani, mwaka 1863, na Papa Leo XIII alikuwa mmoja wa waliokipenda sana.


Pemberton, naye alijitokeza na mchanganyiko wake akifuata mtindo huu lakini yeye hakutumia divai bali alitumia shira.

Baada ya muda kokeini iliacha kutumiwa kwenye vinywaji, baada ya kutambuliwa kama dawa ya kulevya lakini kola ziliendelea kuwa maarufu.

Kwa sasa, viungo pamoja na utaratibu wa kutayarisha soda za Coca-Cola huwa siri kuu, lakini taarifa husema huwa kola hazitumiwi tena. Badala yake, kampuni hiyo hutumia kemikali kuunda ladha sawa na ya kola.

Hata hivyo, jina halijabadilika.
CHANZO BBC

Friday, September 23, 2016

Yahoo yadukuliwa taarifa za watumiaji wake

Mtandao wa Yahoo umethibitisha kuwa wadukuzi wamedukua taarifa za zaidi ya watumiaji milioni mia tano katika akaunti zake za watumiaji.

Hata hivyo Yahoo imesema inaamini kuwa shambulio la kimtandao la mwaka 2014 lilikuwa limefadhiliwa na serikali.

Data zilizoibwa ni pamoja na majina, anuani za barua pepe, namba za simu, tarehe za kuzaliwa na nywila za watumiaji ama (Password). Lakini wadukuzi hao hawakugusa kadi za malipo na taarifa za akaunti za kibenki.

Watumiaji wa mtandao huo wameshauriwa kubadilisha nywila zao (password) zao ili kuepuka udukuzi wa kimtandao.
CHANZO BBC

Madam Rita wa BSS kufilisiwa



MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), kwa kushirikiana na Kampuni ya Udalali ya Yono, wameifungia Kampuni ya Benchmark Productions na kuipa muda wa siku 14, iwe imelipa deni la kodi ya Sh bilioni 7.04, vinginevyo mali za kampuni hiyo zitauzwa kwa mnada.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam Meneja Msaidizi wa Madeni wa TRA, Mkoa wa Kinondoni wa Kodi, Sylver Rutagwelera alisema wamefikia hatua hiyo baada ya kuidai kampuni hiyo inayomilikiwa na Rita Paulsen kwa muda mrefu bila kulipa.

TRA, wakiwa na Kampuni ya Udalali ya Yono, walifika eneo la Mikocheni jijini hapo jana asubuhi ziliko ofisi za kampuni hiyo na kuwaeleza wahusika kuhusu deni hilo, na kuwataka waoneshe risiti za malipo iwapo wameshaanza kulipa deni hilo, jambo ambalo wahusika hao hawakuwa nazo.

Hata hivyo Meneja Operesheni wa Kampuni hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Evelyn alifika ofisini hapo na kuwaambia maofisa hao kuwa walishaanza mawasiliano jinsi ya kulipa deni hilo. “Zipo barua tulizokuwa tumeanza kufanya mawasiliano na TRA, kuhusu deni hili, lakini pamoja na hayo, deni lenyewe ni kubwa kuliko uwezo wa kampuni,” alisema Evelyn.

Hata hivyo Rutagwelera alisema mmiliki wa kampuni hiyo anadaiwa kodi tangu mwaka 2009 na alikuwa akitumia jina lingine kwenye kampuni hiyo na baada ya muda aliifunga na kufungua hiyo ya Benchmark ili hali deni la nyuma hajalipa.

“Mdaiwa huyo alikuwa ana kampuni aliyoipa jina lingine na tulimkumbusha kulipa kodi ya serikali tangu mwaka 2009 ila hakutekeleza na badala yake aliamua kuifunga kampuni na kufungua hii, akidhani deni limefutika”, alisema Rutagwelera.

Alisema baada ya kuona muda unasonga na deni linazidi kuongezeka bila mdaiwa kuonesha juhudi za kulipa waliamua kukabidhi mdaiwa huyo kwa Kampuni ya Yono kwa ajili ya kufuatilia deni hilo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Yono, Scholastika Kevela alisema wameifungia kampuni hiyo na kuanzia sasa walinzi wa Yono watalinda na baada ya muda wa siku 14, waliopewa kulipa deni hilo ukipita, watachukua hatua nyingine kisheria ya kuuza mali za kampuni hiyo kwa mnada.

Alisema deni hilo ni kubwa kwa sababu ni muda mrefu umepita kodi ya serikali haijalipwa na kuwashauri Watanzania kuacha tabia ya kulimbikiza kodi kwa sababu deni litakuwa kubwa ila likilipwa kwa wakati linaondoa usumbufu usio wa lazima.

“Yono tumepewa kazi ya kukusanya madeni ya serikali na tutaendelea kuwakamata wale wote tunaopewa kuwafuatilia lengo sio kuwaumiza ni kuhakikisha kodi ya serikali inakombolewa kwa manufaa ya nchi yetu, kwa maana tunamuunga mkono Rais John Magufuli kuhakikisha taifa letu linaendelea kwa kukusanya mapato stahiki”, alisema Kevela.
CHANZO HABARILEO

Monday, September 19, 2016

Binti wa Donald Trump agwaya maswali mazito ya mwanahabari

Binti wa Donald Trump, mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Chama cha Republican, Ivanka Trump
Binti wa Donald Trump, mgombea uraiswa Marekani kwa tiketi
 ya Chama cha Republican, Ivanka Trump
BINTI wa Donald Trump, mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Chama cha Republican, Ivanka Trump, amelazimika kusitisha mahojiano na gazeti la Cosmopolitan linalochapwa baada ya kuulizwa maswali magumu.
Maswali hayo yanahusu kauli mbalimbali za baba yake huyo alizowahi kutamka kuhusu masuala ya afya ya watoto na likizo ya wazazi.
Badala ya kujibu maswali, binti huyo alimlaumu mwanahabari aliyekuwa akimhoji kwa madai kwamba maswali hayo yamegubikwa na “mambo mengi hasi”.
Binti huyo alikuwa akitaraji kuulizwa kuhusu sera mpya ya afya ya watoto ya mgombea wa Republican Donald Trump, ambayo alisaidia kuiandaa na kuitangaza rasmi wiki hii.
Mwanahabari, Prachi Gupta alimuhoji binti huyo akisema;  “Mwaka 2004 Donald Trump alisema kwamba mimba ni kitu kibaya kwa biashara. Inashangaza kuona sera hii kutoka kwake leo. Unaweza kuzungumzia matamshi hayo na labda ni kitu gani kimebadilika?”
Binti huyo hakuzubaa akajibu; “Sasa nadhani una mambo hasi sana kwenye haya maswali. Kwa mujibu wa gazeti la Cosmopolitan Ivanka akaendelea kulaumu akisema; “Kwa hiyo sifahamu ni kwa kiasi gani inasaidia kutumia muda mwingi na wewe kuhusu hili, kama unatoa matamshi kama hayo.”
Gupta aliendelea; “Ningependa kusema kwamba samahani kwa maswali – unayoyaona kwamba ni hasi. Lakini hayo maswali yana maana kwamba mgombea urais alitoa hayo matamshi wakati fulani. Kwa hiyo mimi nimekuwa nikifuatilia tu.”
Ivanka akajibu; “Ahaa, umesema kwamba alitoa hayo matamshi. Mimi sifahamu kama aliwahi kuyatoa.
Alipooneshwa chanzo cha nukuu ya baba yak ambacho ni ya Donald Trump na Shirika la Habari la NBC mwaka 2004, binti huyo akawa mkali zaidi .
Hasira za binti huyo zilikuwa dhahiri mara alipoulizwa kwa nini hoja za wakati wa kampeni kuhusu likizo haziwahusishi wenza wa mashoga au haijumuishi likizo ya kina baba ya uzazi. Lakini hata hivyo alijibu kwamba sababu ni kuwa “…nia halisi ya mpango ni kuwasaidia kina mama kupona.”
Mwandishi akauliza; “Kwa hiyo nataka kuweka hili sawa, kwa wapenzi wa jinsia moja ambao wanaokubali watoto kuwa wao, ambapo wazazi hao wawili wote ni wanaume, hawatapata likizo maalumu kwa sababu hawahitaji kupona?”
Ivanka Trump akamjibu akisema: “Hayo ni maneno yako, sio yangu. Hayo ni maneno yako. Mpango kwa sasa unaaangalia kina mama zaidi, haijalishi kama watakuwa kwenye ndoa ya jinsia moja au hapana.”
Wakati Gupta alipoanza kumuuliza ni kwa jinsi gani Donald Trump ataweza kugharimia mapendekezo yake ambayo ni ghali sana – kama vile ujenzi wa ukuta kati ya mpaka wa Marekani na Mexico, uwekezaji katika miundombinu na kuongeza matumizi ya kijeshi, Ivanka Trump alijibu kuwa mipango hiyo itagharimiwa na mpango mkuu kabambe wa mageuzi ya kodi kwa nchi hiyo.
Hata hivyo, muda mfupi baada ya hapo alifanya uamuzi ‘mgumu’ wa kusitisha mahojiano hayo. “Naondoka – nalazimika kuondoka. Samahani,” alitamka.
Baadae kwa kupitia ukurasa wake wa Twitter, Ivanka Trump aliandika, “Cosmopolitan, wasomaji wenu wanajali na wanapaswa kujali kuhusu masuala yanayoawaathiri kina mama na watoto. Weka malengo panapostahili – simamia mabadiliko.”
Mtafaruku huo unajitokeza katika wakati ambao tayari timu ya kampeni ya Hillary Clinton, mgombea wa Democrat ikishutumu mpango huo wa Donald Trump kwa madai  kwamba ‘unawaangalia’ kina mama pekee na kuwasahau kina baba.
Imeandikwa na CNN na kutafsiriwa na mwandishi wa Raia Mwema

Tanzania bora duniani huduma za simu na fedha mtandaoni


TANZANIA imetajwa kuwa moja ya nchi zilizoendelea duniani katika matumizi ya huduma za simu na fedha kwa njia ya mtandao.

Hayo yalibainishwa katika mkutano wa kimataifa wa sita wa kujadili namna ya kuboresha zaidi huduma za simu na fedha kwa njia ya mtandao, ulioandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Akifungua mkutano huo Dar es Salaam leo, Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, amesema tangu kuanza kwa matumizi ya huduma za simu na fedha kwa njia ya mtandao mwaka 2008, Tanzania imepiga hatua kubwa katika eneo hilo.
Kwa habari zaidi soma Habarileo Septemba 20.
CHANZO: http://www.habarileo.co.tz/